Kocha wa
timu ya taifa ya Chile Jorge Sampaoli amefikia
makubaliano na shikrikisho la soka nchini humo ANFP kuendelea na kazi yake ya
kukifundisha kikosi hicho hadi mwaka 2018 kwenye fainali za kombe la dunia
zitakazofanyika Urusi.
Sampaoli
mwenye umri wa miaka 54 jana alikuwa na mazungumzo na rais wa shirikisho la
soka la Chile Sergio Jadue waliofikia makubaliano hayo baada ya kocha huyo
kufanya vyema akiwa na timu yao ya taifa kwenye fainali za kombe la dunia mwaka
huu nchini Brazil.
Tovuti ya
shirikisho la soka la nchini Chile imethibitisha makubaliano hayo na Sampaoli
ambaye aliiongoza timu yake hadi kwenye hatua ya 16 bora kwenye
kombe la dunia mwaka huu na kutolewa na
wenyeji Brazil kwa mikwaju ya penalti.
Sampaoli ambaye ni raia wa Argentina alianza
kuifundisha timu ya taifa ya Chile mwaka
2012.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment