Mabingwa wa
ligi kuu ya Ujerumani timu ya Bayern munich imefikia makubaliano na mlinda
mlango wa Liverpool Pepe Reina kwaajili ya kumsajili kama msaidizi wa mlinda mlango namba
moja
Manuel Neuer.
Mwenyekiti wa
Bayern Munich Karl-Heinz Rummenigge amesema Reina
ambaye msimu uliopita aliichezea Napoli ya Italia kwa mkopo anatarji kuwasili
mjini Munich siku chache kutoka sasa kwaajili ya kufanyiwa vipimo na kusaini
mkataba.
Reina ambaye alikuwa mlinda mlango namba mmoja wa Liverpool kwa misimu minane nafasi yake ilianza kuonekana finyu kwenye kikosi cha timu hiyo baada ya kocha Brendan Rogers kumsajili mlinda mlango wa Ubelgiji Simon Mignolet kutoka Sunderland msimu uliopita.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment