Pages

Ads 468x60px

Friday, August 22, 2014

NI KIVUMBI NA JASHO KATIKA NUSU FAINALI ZA MICHUANO YA KAGAME LEO MJINI KIGALI RWANDA.



                   Nyota wa KCCA ya Uganda akiwa dimbani.

 Hekaheka za michuano ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati maarufu kama Kagame intaraji kuendelea leo ambapo michezo miwili ya nusu fainali inatarajiwa kuchezwa mjini Kigali Rwanda uwanja wa Amahoro.
Katika nusu fainali ya awali Polisi na APR zote za nchini Rwanda zitachuana vikali kuwania kufuzu fainali baada ya timu hizo kufuzu hatua hiyo kwa kushinda michezo yao ya robo fainali,ambapo APR iliifunga Rayon Sports na Polisi kuifunga Atletico ya Burundi.
Nusu fainali yapili itakuwa baina ya wababe wa Azam fc timu ya Elmerekh ya Sudan dhidi ya KCCA ya Uganda ambayo iliifunga Atlabara juba ya sudani kusini magoli 3 kwa 1 kwenye hatua ya robo fainali.
Baada ya michezo ya leo fainali ya michuano hiyo inayodhaminiwa na rais wa Rwanda Paul Kagame inataraji kuchezwa tarehe 24 kwenye uwanja wa Amahoro sambamba na pambano la kusaka mshindi wa tatu.

      Polisi fc ya Rwanda itakayokwaana na APR nusu fainali ya michuano ya Kagame mjini Kigali.

    Kikosi cha APR kitakachoivaa Polisi zote za Rwanda katika nusu fainali ya Kagame.

cha timu ya KCCA cha nchini Uganda kitakachoikabili El Merekh ya Sudani kwenye nusu fainali ya michuano ya Kagame leo mjini Kagali.

 Kikosi cha timu ya El Merekh kitakachokabiliana na  KCCA ya Uganda kwenye nusu fainali ya michuano ya Kagame mjini Kigali Rwanda leo.



                                     Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment