Kocha wa mabingwa wa ligi kuu ya
England Manchester City Manuel Pellegrin
amethibitisha kuwa mshambuliaji Edin Dzeco anajiandaa kurefusha mkataba wake
aendelee kubakia katika timu hiyo.
Pellegrin amesema sababu za kumpatia
mkataba mpya mchezaji huyo raia wa Bosnia kunatokana na uzwezo mzuri
aliounyesha msimu uliopita nakusaidia Manchester City kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya
England kwa mara ya pili katika historia.
Pelegrin amemsifia Dzeco aliyesajiliwa
na kocha wa zamani wa timu hiyo Roberto Mancin kwa ada ya paundi milioni 27
akitokea Wolfsburg mwaka 2011 kwakusema
ni mchezaji mhimu ambaye anastahili kuendelea kubaki Manchester City.
Katika michezo 109 aliyocheza kwenye
ligi kuu ya England Dzeco amefunga magoli 46 licha ya mara kadhaa kupata muda
mfupi wa kucheza kutokana na ushindani wa namba katika kikosi hicho.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment