Suarez baada ya kung'ata Chiellini.
Mshambuliaji mpya wa klabu ya Fc
Barcelona ya Hispania Luis Suarez amepunguziwa adhabu yake ya kufungiwa miezi
minne bila kucheza soka na kutocheza mechi nane kwenye timu yake ya taifa ya
Uruguay baada ya rufani yake kusikilizwa leo kwenye mahakama ya kimichezo ya
CAS.
Rufani hiyo iliyosikilizwa leo
nchini Uswis yalipomakao makuu ya shiriukisho la soka duniani Fifa Suarez sasa
ameruhusiwa kufanya mazoezi na klabu yake mpya ya Fc Barcelona lakini adhabu
zake zingine zipo palepale.
Suarez mwenye umri wa miaka 27
ambaye aliadhibiwa na Fifa kutokana na kumng’ata nyota wa timu ya taifa ya
Italia Giorgio Chiellini kwenye fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini
Brazil awali alizuliwa hata kufanya mazoezi na wachezaji wa timu yake mpya
tangu asajiliwe akitokea Liverpool kwa ada ya uhamisho wa paund milioni 75.
Kupunguzwa kwa adhabu hiyo
inamaanisha Suarez atakuwa uwanjani kwa mara ya kwanza akiwa na timu yake ya
Barcelona October 26 wakati ambapo itakuwa ikichana na mahasimu wao wakuwa
katika ligi kuu ya Hispania Real Madrid.
Aidha tofauti na adhabu yake ya
awali amabyo ilimzuia hata kuingia katika uwanja wowote wa soka kwa muda wote
wa adhabu hiyo sasa Suarez anaruhusiwa kushiriki masuala mbalimbali yanayohusu
soka sambamba na kuhudhuria viwanjani pamoja na kufanya matangazo ya lunigha.
YAFUATAYO NI MATUKIO MHIMU YANAYOMHUSU SUAREZ KATIKA MAISHA
YAKE YA SOKA.
April 2013- Aliomba radhi baada ya
kumng’ata mlinzi wa Chelsea raia wa Serbia Branislav Ivanovic na kisha kuadhibiwa
kutocheza mechi 10 za BPL.
|
Dec 2011- Aliadhibiwa kucheza
mechi 8 na faini ya paundi elfu arobaini kwakosa na kumtolea maneno ya
kibaguzi aliyekuwa mlinzi wa Manchester United kwa wakati huo Patrice Evra sasa anakipiga
na Juventus ya Italia.
|
Nov 2010- Aliadhibiwa kutocheza
michezo 7 wakati huo akiwa anaichezea Ajax kwa kosa la kumng’ata nyota wa PSV E indhoven Otman Bakkal.
|
HII NI MICHEZO AMBAYO SUAREZ ATAIKOSA YA MSIMU HUU WA LA LIGA
KATIKA TIMU YAKE MPYA YA FC BARCELONA.
24 August: Elche (H)
|
31 August: Villareal (A)
|
13 September: Athletic Bilbao (H)
|
16/17 September: Champions League
|
21 September: Levante (A)
|
24 September: Malaga (A)
|
28 September: Granada (H)
|
30 September / 1 October: Champions League
|
5 October: Rayo Vallecano (A)
|
19 October: Eibar (H)
|
21 / 22 October: Champions League
|
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment