Mwanariadha wa uingereza Mo Farah ameweka hadharani sababu zilizomfanya ashindwe kushiriki mashindano ya jumuia ya Madola yaliyomazika hivi karibuni mjini Glascow Scotland kwakusema matatizo ya moyo ndiyo chanzo kikuu.
Farah mwenye umri wa miaka 31 amesema tatizo hilo liligundulika alipoanguka bafuni baada ya kutoka kwenye mazoezi mwanzoni mwa mwezi wa tatu mwaka huu na kilichomsaidia ni simu aliyokuwa nayo ambayo aliitumia kumwita mwenzake amsaidie.
Baada ya hapo Farah amesema alikimbizwa hospitali na kukaa siku nne akitibiwa kabla ya kuruhusiwa na kusisitiza kuwa kwa muda wote huo alikuwa akihisi maumivu makali tumboni.
Mshindi huyo wa mbio za mita elfu tano na mita elfu kumi katika mashindano ya Olympic amesema mara baada ya uchunguzi kufanyika iligundulika kuwa kuna kasoro katika mapigo yake ya Moyo.
Farah ambaye kwasasa amepona na amewaomba radhi mashabiki wake wengi waliokuwa wamekata tiketi kushudia michezo ya jumuia ya madola huku akisema kuwa hakutazama mchezo hata mmoja kwenye michuano ya jumuia ya madola.
Kwasasa Farah anajiandaa kushiriki michuano ya European Championships mjini Zurich Uswis ambayo inaanza leo tarehe 12 hadi 17 ya mwezi huu wa nane na anamatumaini makubwa yakurejea uwanjani katika kufukuza upepo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment