Sunday, August 24, 2014
SMAILLING KULAMBA MKATABA MPYA MANCHESTER UNITED.
Chris Smalling.
Klabu ya Manchester United ya Uingereza inajiandaa kufanya mazungumzo na mlinzi wale Chris Smailling kwaajili ya kumpatia mkataba mpya wa miaka mitano majuma machache yajayo.
Mashetani hao wekundu wa Old Traford wamepanga kumwongeza mshahara mchezaji huyo hadi kufikia paundi elfu sabini kwa wiki kama njia ya kumshawishi kubakia klabuni hapo baada ya Arsenal kuanza kumnyemelea.
Mlinzi huyo wa nafasi ya katikati na pembeni kwasasa analipwa mshahara wa Euro elfu sitini na mbili utakaomfanya awe sawa na muingereza mwenzake Phil Jones ambaye wote wanaichezea timu hiyo ya Manchester United.
Wakat huohuo Manchester United imekaribia kumsajili Angel Di Maria kutoka Real Madrid kwa uhamisho wa kati ya Euro milioni 60 hadi 70 baada ya mchezaji huyo kugoma kuongeza mkataba mpya na tayari ameandika waraka kwa mashabiki wa Real akieleza sababu za kuhama Santiago Bernabeu.
Angel di Maria.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment