Kocha mkuu wa timu ya
Manchester City Manuel Pellegrin amethibitisha kuwa kiungo Frank Lampard
anataraji kuanza mazoezi na kikosi chake baada ya kujiunga na mabingwa hao wa
ligi kuu ya England kwa mkopo akitokea New York City ya Marekan.
Pellegrin
ambae ni raia wa Chile amesema kiungo huyo aliyesajiliwa na New York City
akitokea Chelsea atalazimika kupigania namba kwenye kikosi chake hadi hapo
atakaporejea katika ligi kuu ya Marekani
MLS mwezi wa kwanza mwakani.
Kocha huyo
amesema Lampard anataraji kuanza mazoezi na Manchester City jumatano ya wiki
ijayo na atakuwa katika kikosi hicho na kucheza michezo mbalimbali
itakayokuwepo kwenye ratiba yao msimu wa 2014/2015.
Pamoja na
uvumi kuwepo kwamba Lampard husnda asijeze michezo ambayo City itakuwa
ikiikabili Chelsea kocha Manuel Pellegrin amesema hakuna jambo kama hilo kiungo
huyo aliyesajiliwa kwa mkopo wa miezi 6 atacheza kama wachezaji wengine.
Frank Lampard ndani ya uzi wa New York City.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment