Kiungo wa klabu ya Manchester City ya England Samir Nasri amesema anataraji kutangaza hatima yake ya kuichezea timu ya taifa ya Ufaransa au kutoichezea tena katika maisha yake ya soka siku chache zijazo.
Nasri ambaye aliachwa kwenye kikosi
cha Ufaransa kilichoshiriki fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil
amesema tayari ameshafanya maamuzi yake na anataraji kuyatangaza rasmi.
Kiungo huyo ambaye vitendo vya utovu
wa nidhamu ndivyo vilivyomfanya aachwe na kocha mkuu wa Ufaransa Didier
Deschamps ameeleza kuwa suala la kucheza au kutohitaji kucheza kwenye timu ya
taifa atalitangaza katika mahojiano maalumu.
Nasri amesema hajashinda taji lolote
na timu ya taifa jambo ambalo halimpi ugumu wa kutangaza kutoendelea kuichezea
timu yake ya taifa tofauti na kama angekuwa ameshinda mataji mengi lingekuwa jambo
gumu kwake.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment