Rory McIlroy akipokea taji la WGC.
Mcheza Golf Rory McIlroy amejea katika nafasi ya kwanza kwa ubora wa mchezo huo duniani baada ya kufanikiwa kushinda taji la WGC-Bridgestone mjini Ohio akimshinda Sergio Garcia.
McIlroy ameshinda taji hilo la WGC kwa mara ya
kwanza nakumfanya amwengue raia wa Australia Adam Scott kwenye nafasi kwanza
ambayo alikalia tangu mwezi wa tatu mwaka jana.
Akizungumzia ushindi alioupata
Mcllroy amesema anajivunia kupata mafanikio hayo huku akisifu uwezo mkubwa
aliouonyesha nakuahidi kuwa atahakikisha
analinda kiwango chake kidumu msimu huu wote.
Katika hatua nyingine mcheza Golf Tiger Woods yupo kwenye hatari ya kushiriki mashindano
ya PGA nchini Marekani na Ryder Cup mwaka
huu kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya mgongo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment