Pages

Ads 468x60px

Saturday, July 12, 2014

RAIS WA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF JAMAL MALINZI AWASILI MKOANI RUVUMA KWA ZIARA YA SIKU 2.



                         Rais wa Tff Jamal Malinzi.

Rais wa shirikisho la soka nchini Tff Jamal Malinzi leo amewasili mkoani Ruvuma ambapo atakuwa na mazungumzo na viongozi wa chama cha mpira mkoani humo FARU kujadili masuala mbalimbali.
Mwenyekiti wa FARU Golden Sanga amesema ujio wa kiongozi huyo wa ngazi ya juu kwa soka la Tanzania ni wakihistoria na huenda ukaleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo.
Sanga amema mara ya mwisho kwa mkoa wa Ruvuma kutembelewa na uongozi wa juu wa Tff ni miaka ya 1980 ambapo kipindi hicho Tff ilikuwa inajuliakana kama chama cha soka nchini FAT na kiongozi wa mwisho kutoka FAT kutembelea mkoa huo ni Said Elimamri.
Katika ziara hiyo ambayo ni mmoja ya ahadi zake wakati wa kuingia ikulu ya Tff Malinzi atapata fursa ya kuzungumza na wenyeji wake masuala mbalimbali yakimendeleo kwa soka la Ruvuma na nchi kwa ujumla.
Malinzi anataraji kurejea Daresalaam kesho jioni mara baada ya kufunga mashindano ya Sangawane Cup yanayofanyika mjini Songea mkoani Ruvuma ambapo ataota zawadi kwa timu zitakazofanya vyema kuanzia mshindi wa kwanza,wapili,watatu na wanne.
Aidha Malinzi ameahirisha safari yake ya kwenda nchini Brazil kushuhudia fainali ya kombe la dunia hapo kesho baina ya Argentina na Ujerumani kutokana na kubanwa na shughuli mbalimbali ya kiutendaji katika ofisi yake.

                             Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment