Alvaro Morata akiwa na jezi ya Real Madrid.
Mabingwa
wa ligi kuu ya Italia Juventus wamekamilisha usajili wa mshambuliaji Alvaro
Morata kutoka Real Madrid ya nchini Hispania kwa uhamisho wa Euro milioni 20
akikubali kusaini mkataba wa miaka mitano.
Morata
mwenye umri wa miaka 21 jana ijumaa laiwasili
mjini Turin Italia kwaajili ya maandalizi ya kufanyiwa vipimo vya afya
tayari kwakujiunga na vibibi kizee hao wa Turin.
Katika usajili
huyo pande mbili zimekubaliana kuwa kutakuwa na ongezeko la kufikia Euro
milioni 30 kwa Real Madrid endapo nyota huyo ataongezewa mkataba baada ya huu
wa sasa.
Pia mkataba huo utaendelea kuinufauisha Real Madrid kulingana na idadi ya michezo atakayokuwa anacheza chipkizi huyo katika msimu wa 2015/2017 na 2016/2017.
Morata ambaye amefunga magoli 8 katika michezo 23 aliyocheza msimu uliopita akiwa na Reala Madrid anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Juventus akitokea Real Madrid baada ya kiungo Casemiro aliyekuwa kwa mkopo Fc Porto ya Ureno taarifa zilimethibitishwa leo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment