Pages

Ads 468x60px

Saturday, July 12, 2014

BRAZIL KUFA NA KUPONA MBELE YA UHOLANZI LEO KUSAKA MSHINDI WA TATU KATIKA KOMBE LA DUNIA 2014.



                                Kikosi cha timu ya taifa ya Brazil 2014.

Hekaheka za michuano ya kombe la dunia zinataraji kuendelea leo usiku nchini Brazil ambapo wenyeji timu ya taifa ya Brazil watakuwa wakichuana vikali na Uholanzi katika pambano la kusaka mshindi wa tatu.
Timu zote hizi zitakuwa zinaingia uwanjani na maumivu yakudundwa kwenye michezo yao ya nusu fainali ambapo Brazili ililowa mbele ya Ujerumani kwakubugizwa magoli 7 kwa 1 siku chache zilizopita.
Brazil ambayo ilionekana kupwaya baada ya kuwakosa nyota wake wawili mhimu kwenye pambano la nusu fainali nahodha Thiago Silva ambaye alikuwa akitumikia adhabu ya kadi mbili za njano na Neymar ambaye ni majeruhi  leo watakuwa wakifurahia uwepo wa Silva ambaye ameshamaliza adhabu yake.
Tayari nahodha huyo amesema watahakikisha wanaifunga Uholanzi ili kuwafuta machozi mashabiki wao walioumia kutokana na kipigo hicho cha kiistoria walichokipokea kutoka kwa wajerumani.
Neymar ambaye yeye ni majeruhi ataendelea kuwa mtazamaji kutokana na kuumia uti wa mgongo.
Kwaupande wao Uholanzi chini ya kocha mkuu Lois Van Gaan wanaingia uwanjani leo wakiwa na kumbukumbu ya kuondoshwa kwa changamoto ya mikwaju ya matuta na Argentina kwenye pambano la nusu fainali lililochezwa hivi majuzi.
Uholanzi ambayo ilifungwa matuta 4 kwa 2 na kikosi cha Argentina  leo itakuwa ikipigana kufa na kupona kushinda pambano hilo ili kuwapa faraja mashabiki wake ambao wengi waliamini watarejea kumbukumbu yao ya mwaka 2010 ambapo walifungwa na Hispania katika mchezo wa fainali nchini Afrika ya kusini.


                            Kikosi cha timu ya taifa Uholanzi kitakachoivaa Brazil leo.

Wakati matumaini ya Wabrazil yakibakia kwa Oscar katika safu ya ushambuliaji, kwa upande wa uholanzi wataendelea kutegemea majembe yao Arjen Roben na Roben van Persie na wengineo huku kiungo Wesley Sneijder baada ya mkwaju wake kupanguliwa na mlinda mlango wa Argentina Sergio Rumero leo atataka kufuta makosa.
Kesho pazia la michuano hiyo iliyoanza julai 12 mwaka huu litakuwa linafungwa rasmi kwa pambano kali na la kukata na shoka baina ya Ujerumani na Argentina kuanzia majira ya saa 4 kamili usiku kwasaa za Afrika ya mashariki.

     Kikosi cha timu ya Taifa ya Argetina kitakachoikabili Ujerumani kesho katika mchezo wa fainali ya kombe la dunia nchini Brazil 2014.



 Kikosi cha timu ya Taifa ya Ujerumani  kitakachoikabili Argentina  kesho katika mchezo wa fainali ya kombe la dunia nchini Brazil 2014.

                                                                       Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment