Pages

Ads 468x60px

Saturday, July 19, 2014

HATIMAE MWAKALEBELA ATOA ZAWADI KWA TIMU ZILIZOFANYA VYEMA LIGI YA SOKA WILAYA YA IRINGA MJINI.




 
Mdhamini wa ligi ya wilaya ya Iringa mjini Fredrick Mwakalebela.


Katibu mkuu wa zamani wa shirikisho la soka nchini Tff Fredrik Mwakalebela  ameomba kurefusha mkataba wake wa  kudhamini ligi hiyo nakuahidi kuwa na mikakati ya kuifanya ligi hiyo kuwa bora zaidi.
Akizungumza katika hafla ya utoaji wa zawadi kwa timu zilizofanya vyema kwenye ligi hiyo iliyomalizika miezi mitatu iliyopita mjini Iringa Mwakalebela amesema nia yake ni kuona soka linachezwa na vijana kwakuwa michezo ni ajira.
Amesema mpira wa miguu ni mmchezo unaopendwa zaidi dunia na unatoa ajira hivyo kama wadau wataunga kwa pamoja kuzisaidia timu mbalimbali katika wilaya ya Iringa huenda siku za usoni mkoa wa Iringa utaondokana na ukame wa kukosa timu ligi kuu.
Aidha mwakalebela amesema kama atafikia makubaliano na uongozi wa chama cha mpya wilayani Iringa mjini IMDFA juu ya kumpa mkataba mpya atahakikisha anaboresha maslahi ya timu shiriki kwenye ligi ya msimu ujao.
Mwakaleba ameleza sababu kubwa ya kuomba udhamini zaidi  kwenye ligi hiyo uongezwe kubwa zaidi ikiwa hali duni ya kiuchumi ilivyo kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo ambapo mara nyingi zimekuwa zikitembeza bakuli la kuomba misaada hata maji ya kunywa.
Katibu mkuu huyo wa zamani wa Tff hakusita kutoa rai kwa wadau wenye uwezo wa kuendeleza mchezo wa soka na michezo mingine wilayani humo na mkoa wa Iringa kwa ujumla wafanye hivyo ili kuleta maendeleo zaidi.
Kwa upande wake katibu mkuu wa chama cha mpira wilaya ya Iringa mjini Bakari kamtande amesema wapo tayari kurefusha mkataba huo kwakuwa ligi yao ni  yakwanza kupata mdhamini nchini lakini hiyo itakuwa baada ya kuwekana sawa.

Kamtande amechukua nafasi yake kwakuzipongeza timu zote 12 zilizoshiriki kwenye ligi ya msimu huu kwakusema zilionyesha nidhamu ya hali ya juu tofauti na misimu iliyopita kitu ambacho kimeonyesha ni ukomavu wa kifikra kwa viongozi wa timu na wachezaji kwaujumla.
Pia katibu huyo asiye na maneno mengi ametoa pongezi kwa mdhamini wao na kusema licha ya kuchelezwesha zawadi amekamilisha makubaliano yaliyopo kwenye mkataba walioandikishana nae.
Zawadi zilizotolewa na mdhamini  wa ligi hiyo katibu mkuu wa zamani wa Tff Fredrick Mwakalebela ni kama ifuatavyo.
1.Real moja moja ....shilingi laki 5  jezi seti 1,mipira 5 na kikombe chenye thamani ya shilingi laki 6.
2.Mtwivila city…shilingi laki 3,seti 1 ya jezi  na mipira 3.
3.Mtwa fc…shilingi laki 2,jezi seti 1 na mipira 2.
Nimu ya nidham zima moto…shilingi laki 1, seti 1 ya jezi na mpira1.
Mfungaji bora. Ni Endru chanungu maarufu kama  Ambani  wa mtwivila city  amezawadiwa shilingi elfu 80.



 katibu mkuu wa chama cha soka Iringa mjini Bakari Kamtande.

mwenyekiti wa chama cha soka Iringa mjini Ramadhani Mahano.

 
wawakilishi wa timu mbalimbali zilizoshiriki ligi ya wilaya msimu huu.



waandishi wa habari pia hawakuwa nyuma wakiongozwa na Denis Nyari wa Overcomers radio mwenye koti lenye rangi ya damu ya mzee.

           Kombe la bingwa wa ligi hiyo timu ya Real Mojamoja


                     Mwakalebela kabla ya kugawa zawadi.
                   Jezi na mipira kabla ya kugawiwa kwa timu.
                                Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment