Pages

Ads 468x60px

Monday, July 14, 2014

SCOLARI AWASILISHA BARUA YA KUJIUZULU NAFASI YAKE.




                                             Scolari.

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil Luiz Felipe Scolari amewasilisha barua ya kujiuzulu nafasi hiyo kwa uongozi wa shirikisho la soka nchini humo FA (CBF) baada ya kushindwa kumaliza vyema fainali za kombe la dunia zilizomalizika usiku wa kuamkia leo na Ujerumani kuwa bingwa.

Scolari mwenye umri wa miaka 65 amelazimika kufikia uamuzi huo baada ya kushindwa kutwaa ubingwa wa dunia akiwa na kikosi hicho cha Brazil licha ya kufanya hivyo mwaka 2002 na katika michezo 29 ameshinda michezo 19 pekee kwenye awamu ya pili akiwa anainoa Brazil.

Pamoja na kuvuka hatua ya makundi na kufika nusu fainali ya kombe la dunia mwaka huu Brazil ilikumbana na kipigo cha michezo michezo miwili mfululizo kilichovunja rekodi ya taifa hilo kupoteza mipambano miwili takribani miaka 39 iliyopita.

Kipigo hicho ambacho kimeingia kwenye historia ya taifa hilo ni kile cha magoli 7 kwa 1 ambapo ilikipokea kutoka kwa Ujerumani hatua ya nusu fainali kabla ya kufungwa na Uholanzi magoli 3 kwa 0 kwenye pambano la kusaka mshindi wa tatu.

                                          Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment