Mshambuliaji
wa timu ya Manchester City,Alvaro Negredo anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa
miezi kadhaa kutokana na kuumia mguu wa kulia kwenye mchezo wa kirafiki dhidi
ya hearts.
Negredo
mwenye umri wa miaka 28 amethibitisha taarifa hizo kupitia mtandao wake wa
kijamii wa Instagram akiambatanisha pamoja na picha ya mguu huo wenye majeraha.
Nyota huyo
amewataka mashabiki wa Manchester City
kutokuwa na hofu juu yake katika kipindi hiki kigumu ambacho atakuwa nje ya
uwanja kwa mda mrefu.
Taarifa hizo
zitakuwa ni mbaya kwa Kocha wa kikosi hicho, Manuel pellegrin wakati
wakijiandaa kutetea ubingwa wao wa ligi kuu England kwa msimu unao kuja.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment