Angel Di Maria.
Licha ya kuwepo kwa taarifa mbalimbali zinazomhusisha nyota wa Real Madrid
Angel Di Maria kuihama timu hiyo kocha Carlo Ancelotti amesema mchezaji huyo bado
yupo kwenye mipango yake msimu ujao.
Ancelotti amesema Di Maria mwenye
umri wa miaka 26 bado ni mchezaji wa
Real Madrid na klabu hiyo itaendelea vizuri
na masuala yake ya uhamiso hadi siku yake ya mwisho akiwa Santiago Bernabeu.
Kocha huyo raia wa Italia
amesema baada ya ujio wa wachezaji wawili wapya msimu huu wa usajili kikosi
chake kimeimarika na kuwa cha ushindani kuliko msimu uliopita.
Di Maria ambaye alijiunga na
Real Madrid mwaka 2010 akitokea Benifica ya Ureno amekuwa akihusishwa na
mipango ya kuhamia PSG ya Ufaransa na pia Manchester United ya Uingereza nayo
imekuwa ikitajwa kumwania mchezaji huyo raia wa Argentina.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment