Pages

Ads 468x60px

Saturday, July 19, 2014

BORINI HUYOOOOOOO SUNDERLAND KWA DAU LA PAUND MILIONI 14.


                 Fabio Borini akiwa na ndani ya uzi wa Liverpool.

Timu ya Liverpool imefikia makubaliano  ya kummuza  mshambuliaji Fabio Borini kwenda  Sunderland kwa uhamisho fa paundi milioni 14.
Borini mwenye mwenye umri wa miaka 23 alikuwa Sunderland  kwa mkopo msimu uliopita  na kuisaidia timu hiyo kukwepa janga la kushuka daraja.
Katika msimu uliopita raia huyo wa Italia alikwamisha kimiani magoli 10 na kunyakua tuzo ya mchezaji bora chipkizi wa timu hiyo kwa msimu huo.
 Licha ya nyota huyo kupigania namba kwenye kikosi cha Liverpool na kufunga magoli 2 msimu wa 2012/2013 haikutosha kumshawishi kocha Brendan Rodgers jambo liliofanya atolewe kwa mkopo kwenda Sunderland.
 Borini alikuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na kocha Brendan Rodgers kutoa Roma ya Italia kwa dau la paundi milioni 11 mwezi july mwaka 2012.
 Mbali na kuinusuru Sunderland isishuke daraja msimu uliopita Borini aliiwezesha Sunderland kufikia hatua ya fainali kwenye kombe la Capital one licha ya kikosi hicho kufungwa na Manchester City kwenye fainali.
 Kama atajiunga na Sunderland mmoja kwa mmoja Borini atakuwa mchezaji wa 4 kusajiliwa msimu huu baada ya kiungo Jordi Gomez kutoka Wigan,mlinzi Billy Jones kutoka West Brom na mlindamlango Costel Pantilimon kutoaka Manchester City.


                 Mkule.blogsport.com


3 comments:

  1. Liverpool wamepoteza jembe.

    ReplyDelete
  2. Kweli kama aliisaidia Sunderland isishuke daraja huyo alikuwa mtu mhimu sana kusalia Liverpool.

    ReplyDelete
  3. Acha aende zaje tutapata jembe ligine kali zaidi yake.

    ReplyDelete