Arturo Vidal
Maombi ya
mashabiki wa Manchester Unite kuwa na nyota wa Juventus Arturo Viadl msimu ujao
huenda yakawa yanakaribiwa kujibiwa na mungu baada ya mchezaji huyo raia wa
Chile kuweka wazi kwamba hadhani kama atakuwepo Italia msimu ujao.
Kiungo huyo
ambaye amekuwa akifukuziwa kwa karibu na Manchester United amekaririwa na
gazeti moja la nchibni Chile lijulikanalo kama
La Cuarta akisema ni vigumu kuzungumzia timu kubwa ukiwa ndani
ya klabu yenye mafanikio kama Juve ambayo ameshinda mataji 3 ya ligi kuu ya Italia.
kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 amesema anaziheshimu timu ambazo zimeonesha nia ya kutaka kumsajili Real Madrid na Manchester United lakini juu ya maombi yao anayeweza kuvizungumzia ni wakala wake ambaye ndiye msimamizi wake.
Nyota huyo
ambaye alisajiliwa na Juventus mwaka 2011 kwa Euro milioni 10.5 kutoka Bayer
Leverkusen amesema hadi sasa hajui kama atabakia katika timu yake na mara baada
ya kurejea Italia akitokea kwao Chile ataonana na kocha mpya Massimiliano
Allegri kuona kipi kitafuata.
Hii ni kauli
yake aliyoitoa…"I honestly do not know if my cycle with Juventus is
finished. When I return to Italy I will talk with the new coach and see what
happens.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment