Jose Mourinho.
Baada ya aliyekuwa
mshambuliaji wa timu ya Chelsea Romelu Lukaku kujiunga na Everton kocha Jose
Mourinho amesema mchezaji huyo hakuwa tayari kupigania namba kwenye kikosi
hicho cha jijini London.
Mourinho ameeleza sababu ya
kuruhusu mchezaji huyo yaia wa Ubelgiji kuondoka Stanford Bridge kuwa Lukaku
alitaka kuchezea Chelsea na awe chaguo la kwanza jambo ambalo ni gumu kwenye
kikosi chake.
Kocha huyo raia wa Ureno amezidi kutetea uamuzi wa kumuuza nyota huyo
kwakusema baada ya Everton kupeleka dau zuri wamelazimika kummuuza mchezaji
huyo ili klabu inufaike kwa kupata fedha za kuwasaidia.
Lukaku ambaye amejiunga na
Everton maarufu kama Toffiz kwa uhamisho ulioweka rekodi kwa wachezaji wenye
umri wa miaka 21 alifunga magoli 15 msimu uliopita wa ligi katika klabu hiyo akitokea
Chelsea kwa mkopo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment