Mabingwa wa ligi kuu ya
Hispania timu ya Atlertico Madrid imerefusha makataba wake na kampuni ya kimarekani
ya Nike inayojishughulisha na utengenezaji wa vifaa vya michezo hadi mwaka
2026.
Taarifa zilizothibitishwa zimemkariri rais wa timu hiyo Miguel Angel
Gil Marin akisema wanashukuru kuendelea na mkataba mrefu zaidi na kampuni hiyo na hilo ni jambo
mhimu sana kwao.
Kwa mara ya kwanza kampuni ya
Nike kuingia makubaliano ya kutengeneza
vifaa vya michezo na klabu hiyo ilikuwa mwaka 2001 na mkataba huu mpya
utaifanya Nike ifikishe miaka 25 na rais wa Atletico Madrid amesema hayo ni mafanikio kwao.
Katika msimu uliopita wa La
liga timu ya Atletico Madrid chini ya kocha Diego Simeoni ilitwaa ubingwa wa
ligi hiyo ya Hispania kwa mara ya kwanza
tangu mwaka 1996.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment