Ba akishangilia goli kwa imani ya dini yake ya Kiisilaam.
Mshambuliaji
wa Chelsea raia wa Senegal Demba BA amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Besiktas
klabu hiyo ya Uturuki na mchezaji mwenyewe wamethibitisha.
Ba mwenye
umri wa miaka 29 katika kipindi cha miezi 18 amefunga magoli 14 kwenye michezo
51 aliyoichezea Chelsea maarufu mama The Blues tangu ajiunge nayo mwezi wa
kwanza mwaka jana akitokea Newcastle United.
Besiktas
inayoshiriki ligi kuu ya Uturuki imethibitisha usajili huo kupitia tovuti yake
huku Demba Ba akithibitisha kuhamia kwenye kikosi hicho kupitia ukurasaa wake
wa Twita.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment