Robert Pires akiwa na jezi ya timu ya taifa ya Ufaransa.
Licha ya
umri kumtupa mkono nyota wa zamani wa klabu ya Arsenal Robert Pires
amethibitisha kuwa ataendelea kucheza soka katika ligi kuu ya nchini India
maarufu kama Super League (ISL).
Peres ambaye
mwezi wa kumi mwaka huu atafikisha umri wa miaka 41 hajawahi kucheza soka tangu
aachane na klabu ya Aston Villa miaka mitatu iliyopita na mchezaji huyo amesema
anajisikia furaha kuccheza mpira kwenye ligi hiyo ya India.
Hatahivyo
mchezaji huyo aliyewahi kushinda kombe la dunia mara mmoja akiwa na timu ya
taifa ya Ufaransa hajaweka wazi ni timu ipi atakayoenda kuichezea akiwa nchini
India.
Kutakuwepo na
mashindano mapya nchini India yakishirikisha timu nane kuanzia mwezi wa kumi
hadi wa kumi na mbili mwaka huu.
Robert Pires akiwa na jezi ya timu ya Arsenal.
Robert Pires akiwa na jezi ya timu ya Aston Villa.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment