Pages

Ads 468x60px

Tuesday, July 15, 2014

CBF YATHIBITISHA SCOLARI NA WAPANGA KONI WAKE KUACHIA NGAZI.



                                     Luiz Felipe Scolari.

Uongozi wa shirikisho la soka nchini Brazil CBF umethibitisha kwamba aliyekuwa kocha mkuu wa timu ya taifa hilo Luiz Felipe Scolari amejiuzulu nafasi yake.

Taarifa hiyo imesema Scolari na wasaidizi wake wote wameachia ngazi kwakujiuzulu kufuatia matokeo mabovu kwenye michezo yao miwili ya mwisho waliyocheza katika fainali za mwaka huu za kombe la dunia zilizomalizika juzi.

Makamo wa raisi wa shirikisho hilo la soka nchini Brazil Marco Polo del Nero amesema wanamshukuru Scolari na wasaidizi wake kwa mchango walioutoa kwenye timu ya taifa licha ya kutopata matokeo waliyoyatarajia.

Scolari aliyewahi kuifundisha timu ya taifa ya Ureno pamoja na klabu ya Chelsea ya nchini England jana aliwasilisha barua katika ofisi za shirikisho la soka nchini Brazil ya kujiuzulu nafasi hiyo licha ya mkataba wake ulikuwa unamalizika mara baada ya kuisha kwa fainali za kombe la dunia.

Katika fainali za mwaka huu ambapo ubingwa umeenda kwa Ujerumani baada ya kuifunga Argentina katika hatua ya fainali goli 1 kwa 0 Brazil ya Scolari iliambilia nafasi ya nne kufuatia kipigo cha magoli 3 kwa 0 ilichokipata kutoka kwa Uholani.

Kwenye mchezo wa kusaka mshindi wa tatu  Brazil hiyo hiyo ikiweka rekodi kwa kufungwa magoli mengi zaidi katika mchezo mmoja ambapo ilinyukwa magoli 7 kwa 1 na Ujerumani katina nusu fainali.

                       Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment