Wakala wa Yaya Toure amedai kuwa sababu ya kiungo huyo wa Manchester
City kutoshinda tuzo zozote kubwa ni kutokana na rangi ya ngozi yake.
Wakala huyo, Dmitri Seluk amesema kiungo huyo raia wa Ivory
Coast angeweza kumaliza katika nafasi ya juu zaidi ya nafasi ya tatu katika
tuzo za PFA na FWA za mchezaji bora wa mwaka, na pia zaidi ya nafasi ya 12
katika tuzo ya Ballon d'Or, kama angekuwa mzungu.
Luis Suarez alishinda tuzo ya PFA na FWA akifutiwa na Eden Hazard na Steven Gerrard katika kura zilizopigwa.
Luis Suarez alishinda tuzo ya PFA na FWA akifutiwa na Eden Hazard na Steven Gerrard katika kura zilizopigwa.
Seluk ameongeza kusema: "Amesikitishwa kidogo na hali ilivyo.
Messi ni mchezaji mzuri katika historia ya soka na ninawaheshimu sana Ronaldo
na Ribery. Yaya anawaheshimu wachezaji hao. Lakini ni vigumu kwa Mwafrika
katika tuzo hizi. FIFA inahitaji kubadilisha kitu hapa."
Seluk pia amekataa kuhakikisha kuwa Yaya atakuwepo City msimu ujao, akisema: "Kama klabu kubwa kama PSG au Real Madrid wakipanda dau kubwa, Man City watalazimika kuamua kitakachofuata."
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment