Kiungo wa kimataifa wa Ivory
Coast na klabu ya Manchester City Yaya Toure amebainisha kuwa anataka
kuitumikia timu hiyo kwa muda mrefu kadri ya itakavyowezekana.
Yaya Toure.
Yaya mwenye umri wa miaka 31
amesema anafuraha kubakia kwa mabingwa hao wa ligi kuu ya England na hasa baada
ya kujiunga na timu hiyo inayojiandaa na msimu mpya wa 2014-2015.
kiungo huyo ambaye hapo
awali alikuwa akihusishwa na mipango ya kujiunga na PSG ya Ufaransa amewataka
mashabiki wa Manchester City kutoamini maneno yasiyotoka kwenye kinywa chake
lakini yatakayozungumzwa na wakala wake ni ya kweli.
Toure ambaye ni miongoni mwa
wachezaji walioiwezesha City kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Enfglannd msimu
uliopita amesema anajisikia furaha kuungana na wenzaje kwenye maandalizi ya msimu
mpya chini ya kocha Manuel Pellegrini.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment