Lahm aliyeshikilia kombe la dunia.
Kiungo wa mabingwa wa ligi
kuu ya Ujerumani Bayern Munich Philpp Lahm ametangaza kustaafu kichezea timu ya
taifa lake la Ujerumani ambao ni mbabingwa mara nne wa kombe la dunia.
Uamuzi wa Lahm mwenye umri
wa miaka 30 kutangaza kustaafu kuitumikia timu ya taifa umewashtua wengi ikiwa
ni siku chache baada ya Ujerumani kutwaa ubingwa wa dunia kwakuifunga Argentina
goli 1 kwa 0 katika hatua ya fainali nchini Brazil.
Kiungo huyo ambaye
ameiongoza vyema Ujerumani kutwaa taji kubwa la kwanza tangu mwaka 1996 ambapo
nchi hiyo ilinyakua ubingwa wa mataifa ya Ulaya amesema amemtaarifu kocha
wa timu ya taifa Joachim Low juu ya
uamuzi wake huo.
Nahodha huyo ambaye hucheza
nafasi ya ulinzi wa pembeni kwenye timu yake ya taifa amecheza michezo 113 na kuwa mchezaji wa 4
aliyecheza michezo mingi zaidi kwenye kikosi hicho nyuma ya Lothar Matthaus michezo
150, Miroslav Klose michezo 137 na Lukas Podolski michezo 116.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment