Dejan Lovren.
Baada ya klabu ya Liverpool kufikia
makubaliano ya kumsajili mlinzi wa Southampton Dejan Lovren,mchezaji huyo
anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya mwishoni mwa wiki hii.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka
25 anatarajiwa kufanyiwa vipimo hivyo kabla ya Liverpool kurejea Anfield
wakitokea kwenye ziara yao nchini Marekani ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi
kuu England.
Lovren ambaye ni mchezaji wa
kimataifa wa Chile ameeleza kuwa anafurahia kwenda kuichezea timu hiyo huku
akiamini ni muda muafaka wa kukamilisha ndoto zake za muda mrefu katika soka.
Liverpool mpaka hivi sasa
wamewasajili wachezaji wanne akiwemo Rickie Lambert na Adam Lallana kutoka
Southampton, mchezaji Emre Can wa Bayer Livakuzen pamoja na Lazar Markovic wa
Benfica.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment