Arturo Vidal
Uongozi wa mabingwa wa ligi
kuu ya Italia Juventus umezitolea uvivu timu zinazo winda saini ya mchezaji wao
Arturo Vidal.
Taarifa kutoka ndani ya
uongozi wa Juve zimejuza kuwa licha ya kupokea maombi kutoka vilabu mbalimbali
barani Ulaya vikimhitaji raia huyo wa Chile wao hawana mpango wa kumuuza ntota
huyo.
Mkurugenzi wa michezo wa
Juve Giuseppe Marotta amesema hawajawahi
kufikiria kumpiga bei mchezaji huyo na hadi sasa hawana nia ya kumpeleka sokoni
mpachika mabao huyo mahiri.
Taarifa hizi ni mbaya kwa
Manchester United ambayo imekuwa ikiimarisha mbio zake za kunasa sahihi ya myoa
viduku huyo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment