Timu ya Fc
Barcelona imethibitisha kufikia makubaliano ya kumsajili mchezaji Jeremy
Mathieu raia wa Ufaransa kutoka Valencia kwa dau la Euro milioni 20 na kupewa mkataba wa miaka minne.
Barcelona imekuwa
katika mawindo ya usajili kwa muda mrefu ikimtafuta mlinzi wa kati kuziba
nafasi iliyoachwa wazi na Carles Puyol aliyestaafu soka mwishoni mwa msimu
uliopita na Mathieu mwenye umri wa miaka 30 amekuwa mbadala wake.
Fc Barcelona
imethibitisha kupitia tovuti yake kwamba
imefikia makubaliano na Valencia
kumsajili raia huyo wa Ufaransa
anajiandaa kusaini mkataba wake wa miaka 4 na manunuzi yake ni Euro
milioni 20 lakini thamani yake itakuwa Euro milioni 50.
Mathiew alianzia
soka lake katika timu ya Sochaux lakini pia amewahi kuvaa jezi ya Touluse kabla
ya kujiunga na Valencia msimu wa 2009
akicheza michezo 177 na kufunga magoli 7 kwenye kikosi hicho.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment