Andy Carroll.
Mchezaji wa timu ya West Ham Andy
Carroll,anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa miezi mnne kufuatia kupata majeraha
ya goti wakiwa ziarani kujiandaa na ligi kuu Enland.
Carroll, leo atafanyiwa upasuaji
katika mguu wake wa kushoto sehemu ya goti baada ya kuumia wakati wakiwa kwenye
ziara yao nchini Uholanz ya kujiandaa na msimu mpya unao kuja.
Hata hivyo si mara ya kwanza kwa mchezaji
huyo kupata majeraha kama hayo akiwa na kikosi hicho kwani mwaka 2012 mwezi wa
10 alikaa nje ya uwanja mwezi mmoja kutokana na majeraha ya goti.
Taarifa kutoka katika tovuti ya West
Ham imeeleza kuwa wamepata pigo kubwa baada ya mchezaji huyo kupata majeraha
hayo huku bado wakiendelea kuwa na matumaini ya kurejea mapema kwa nyota huyo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment