Tayari jezi ya nyota mpya wa Real Madrid Jemes Rodriguezi ipo sokoni.
Klabu bingwa
barani Ulaya Real Madrid leo imetangaza rasmi kukamilisha usajili wa
mshabuliaji Jemes Rodriguez kutoka Monaco ya Ufaransa kwa kiasi cha Euro
milioni 88 kwa mkataba wa miaka sita na
kupewa jezi namba 10.
Madrid
ambayo hivi karibuni imekamilisha uhamisho wa kiungo Ton Kroos kutoka Beryn
Munich ya Ujerumani imetangaza kupitia tovuti yake kuwa imekamilisha usajili wa
raia huyo wa Colombia baada ya kufaulu vipimo vya Afya.
Rodriguez ambaye
alijiunga na Monaco mwaka jana akitokea Fc Porto ya Ureno kwa ada ya Euro
milioni 45 mkataba wake utamalizika mwaka 2020 msimu uliopita alifunga magoli 9
katika michezo 34 aliyocheza akiwa na Monaco.
Rodriguez mwenye umri wa miaka 22 alianzia soka lake katika klabu ya Envigado na katika fainali za kombe la dunia mwaka huu aliisadia Colombia kuingia robo fainali kabla ya kuondoshwa na Brazil na huku yeye akiibuka mfungaji bora kwa kufunga magoli 6.
Hapa Rodriguez akiwa na Cristiano Ronaldo.
Hapa Jemes Rodriguez akisalimiana na kocha Carlo Ancelotti.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment