Pages

Ads 468x60px

Saturday, July 12, 2014

MBASPO ACADEMY KUIKOSA MICHUANO YA ROLLING STONE KUTOKANA NA UKATA WA FEDHA.






                           kikosi cha Mbaspo academy cha mkoani Mbeya.

Timu ya soka ya Mbaspo academy ya mkoani Mbeya imekwama kushiriki mashindano ya Rolling stone yanayotaraji kuanza tarehe 15 ya mwezi huu jijini Daresalaam.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo ya kulea na kukuza vipaji vya soka nyanda za juu kusini mwa Tanzania Haroub Suleiman amesema jitihada zao za kushiriki zimeshindikana licha ya juhudi kadhaa walizozifanya.

Haroub ambaye ni katibu mkuu wa chama cha kandanda mkoani Mbeya amesema hadi kufikia jana walikuwa na kiasi cha shilingi milioni 4 pekee kati ya milioni 8.5 ambazo zinahitajika kwaajili ya gharama ya safari na chakula na malazi.

Mkurugenzi huyo ambaye amekuwa mstari wa mbele kuhamasisha soka la vijana kupitia taasisi hiyo yenye makazi yake makuu mjini Mbeya amesema kama watapata mdhamini wa kuwasaidia kiasi kilichopungua wapo tayari kuondoka kwenda jijini Daresalaam kushiriki michuano hiyo.

Amebainisha kuwa kikosi cha Mbaspo kwasasa kinaendelea kujifua kwaajili ya mashindano mbalimbali ambayo wamekuwa wanaalikwa na wachezaji wanamorali kubwa ya kucheza soka.

Mkurugenzi wa Mbaspo academy Haroub Suleiman.(aliyesimama katikakati)

Wakati huo huo timu ya Ruaha academy ya mkoani Iringa ambayo tayari ipo jijini Daresalaam kwaajili ya kushiriki mashindano ya Rolling stone imeendelea kujifua na leo imecheza mchezo wa kirafiki na timu ya Tabata Future nakufanikiwa kushinda magoli 4 kwa 0.

Michuano ya Rolling stone ambayo hufanyika kila mwaka kwakushirikisha mataifa mbalimbali ya ukanda wa Afrika mashariki na kati inaanza kutimua vumbi tarehe 15 ya mwezi huu wa 7 jijini Daresalaam.
Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment