Afisa habari na mawasiliano wa Tff, Bonifasi Wambura.
Viingilio
kwa mechi ya Taifa Stars na Msumbiji itakayochezwa keshokutwa (Jumapili) Uwanja
wa Taifa jijini Dar es Salaam ni sh. 7,000 na sh. 30,000 kwa viti maalumu 4,500
tu.
Kuanzia
kesho asubuhi (Jumamosi) tiketi za kielektroniki zitauzwa pia katika magari
maalumu kwenye vituo vya Buguruni Shell, Dar Live Mbagala, Ferry Magogoni,
Kigamboni, OilCom Chang’ombe, OilCom Ubungo, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa
(Kariakoo), TCC Club Chang’ombe na Uwanja wa Taifa.
Aidha
tiketi zinapatikana kupitia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha bonyeza 4,
bonyeza tena 4 kisha weka namba ya kampuni 173399 kisha ingiza 7000 kama namba
ya kumbukumbu ya malipo, kisha andika tena 7000 kwenye weka kiasi, kasha weka
namba ya siri na baadaye bonyeza 1 kukubali.
Utapokea
ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo vya kuchukua tiketi ukiwa na namba
ya uhakiki wa malipo yako.
Vituo
vya MaxMalipo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa
Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata
Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illussions (Millennium Tower
na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta
na Upanga).
Vodashop
(Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station
(Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol
Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City
Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na Uwanja wa Karume.
SEMINA
ELEKEZI AIRTEL RISING STARS
Semina
elekezi ya michuano ya Airtel Rising Stars kwa mikoa sita inafanyika kesho
(Julai 19 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam.
Washiriki
wa semina hiyo ni kutoka mikoa ya Mbeya (Katibu na mwakilishi wa wanawake),
Mwanza (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Morogoro (Katibu), Ilala (Katibu na
mwakilishi wa wanawake).
Temeke
(Katibu na mwakilishi wa wanawake), Kinondoni (Katibu na mwakilishi wa
wanawake), Dar es Salaam (Mwenyekiti na Katibu), na Chama cha Mpira wa Miguu
Zanzibar (ZFA) kitakachowakilishwa na mwakilishi wa wanawake.
Washiriki
wengine katika semina hiyo ambayo mgeni rasmi atakuwa Katibu Mkuu wa TFF,
Mwesigwa Selestine ni wajumbe wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana ya TFF.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment