Mshambuliaji wa timu ya taifa ya
Uganda Emmanuel Okwi ameondolewa katika kambi
ya kikosi hicho kinachojiandaa kucheza mchezo marejeano dhidi ya Mauritania kuwania tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika
mwakani.
Okwi ambaye anaichezea
Yanga ya jijini Dare-salaam ataukosa
mchezo huo unaotaraji kuchezwa tarehe 3 ya mwezi ujao kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyonga timu ya Uganda Creans Milutin Sredojevic ‘Micho’
amethibitisha.
Mshambuliaji huyo
alitolewa kipindi cha pili katika mchezo wa awali ambapo Uganga ilishinda magoli
2 kwa 0 pambano lililochezwa katika uwanja wa Nelson Mandela uliyopo Namboole
nchini Uganda.
Wachezaji wa Uganda Creans
wanaocheza soka nchini Kenya Godfrey Walusimbi na Geoffrey Kizito wa Gor mahia
na nyota wa Tusker fc Khalid Aucho wamejiunga na wenzao kambini jana usiku tayari kwa safari ya Alhamisi ya wiki hii
kuelekea Mauritania.
Nyota wa Uganda Creans waliopo kambini hadi sasa ni : Benjamin Ochan, Robert Odongkara, Denis Iguma, Nicholas Wadada, Denis Okot, Savio Kabugo, Richard Kassaga, Andrew Mwesigwa, Isaac Isinde, Kyambadde, Farouq Miya and Brian Majwega, Godfrey Walusimbi, Geoffrey Kizito, Robert Ssentongo, Brian Umony and Hamis Kizza.
Mkule.blosport.com
No comments:
Post a Comment