BINGWA wa ngumi za super
middle Weight bondia Francis Cheka maarufu kwa jina la SMG amesomewa
shitaka linalomkabili katika mahakama ya hakimu mfawidhi mkoa wa morogoro juu ya
kufanya shambulizi la aibu kwa meneja wake wa baa ndg.Bahati
Kabanga mjini Morogoro.
Akisoma shitaka hilo Mwendesha
mashitaka Bi Aminatha Mazengo amesema kuwa Cheka anakabiliwa na shitaka la
shambulio la aibu ambapo anashitakiwa kwa mujibu wa kifungu namba miambili
arobaini na moja( 241)kifungu cha kumi na sita (16) cha mwaka elfumbili na
mbili (2002) cha makosa ya jinai
Na kuwa mnamo tarehe mbili mwezi wa
saba mwaka elfumbili na kumi na nne maeneo ya ukumbi wa vijana social Mjini
Morogoro bila ya halali alimshambulia Bw Bahati.
Cheka amekana shitaka hilo na
hivyo Hakimu anayesimamia kesi hiyo Bw Said Diwani Msuya amesema kuwa
dhamana kwa mshitakiwa iko wazi kwa wadhamni wawili ambapo kila mmoja ametakiwa
kuwa na dhamana ya shilingi Millioni moja .
Kesiu hiyo imehirishwa hadi tarehe
ishirini na tatu mwezi wa saba mwaka elfumbili na kumi na nne.
Hapa Cheka akiwa Ulingoni(mwenye bukta nyekundu.)
Hapa Cheka akiwa Ulingoni(mwenye bukta nyekundu.)
mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment