Pages

Ads 468x60px

Tuesday, July 22, 2014

BRAZIL YARUDIA MATAPISHI,YAMPA DUNGA MIKOBA YA SCOLARI.



                                               Dunga.

Shirikisho la soka nchini Brazil CBF limiethibitisha kuwa Dunga ndiye kocha mpya wa timu yao ya taifa kuchukua mikoba ya Luiz Felipe Scolari aliyeachia ngazi hivi karibuni kufuatia kikosi ncha nchi hiyo kushindwa kutwaa ubingwa wa kombe la dunia mwaka huu.
Ndunga ambaye alifanikiwa kushinda kombe la dunia mwaka 1994 akiwa nahodha wa Brazil kuteuliwa kwake itakuwa mara ya pili kuifundisha timu ya taifa hilo maarufu kama Selecao baada ya kuwahi kuinoa timu hiyo kati ya mwaka 2006 -2010.

Dunga mwenye umri wa miaka 50 mara baada ya kuthibitishwa kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Brazil amesema bado Brazil inauwezo wa kushindana  na kutwaa mataji na anaamini wataonyesha ubora wao.

Mlinzi huyo wa zamani wa Brazil amesema hawapaswi kufikiria kwamba walikuwa bora bali wao ni bora hadi sasa  kwasababu wanavijana wengi wenye vipaji vikubwa  na yapo mataifa yanayotamani kuwa na timu kama ya Brazil.

Dunga amesema mchezo wa mpira wa miguu sio mchezo wa mtu mmoja au watu wawili maarufu  bali unahitaji ushirikiano wa wachezaji wote katika timu.

Katika maisha yake ya soka Dunga amewahi kuichezea timu ya taifa ya Brazil michezo 60 akishinda michezo 42 na kikosi hicho  huku kikosi chao kikifungwa michezo 6 pekee.

Licha ya kushinda kombe la Copa America mwaka 2007 na kombe la mabara mwaka 2009 akiwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil Dunga alikosolewa sana kabla ya kutimuliwa  mwaka 2010  baada ya kufungwa na Uholanzi hatua ya robo fainali.

Baada  ya uteuzi wa kocha huyo mpya kikosi cha kwanza cha timu ya taifa ya Brazil kinaraji kutangazwa mwishoni mwa mwezi wa 8 mwaka huu kabla ya kuikabili Colombia,na Ecuador nchini Marekani.

Dunga baada ya Brazil kutwaa kombe la dunia 1994.

Dunga akiwa na kikosi cha Brazil kwenye fainali za kombe la dunia mwaka 2010 nchini Afrika ya Kusini.

                             Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment