Walcott akitolewa uwanjani kwa machela.
Wakati msimu
mpya wa ligi kuu ya England ukitaraji kuanza mwezi ujao mshambuliaji wa pembeni
wa timu ya Arsenal Theo Walcott yupo
mbioni kurejea uwanjani baada ya kukosa michezo ya mzunguko wa pili wa ligi hiyo msimu uliopita.
Walcott
ambaye aliumia msimu uliopita kwenye mchezo dhidi ya Tottenham ambapo Arsenal
ilishinda magoli 2 kwa 0 amesema kwasasa anaendelea kupona vizuri na
anamatumaini ya kuanza msimu mpya akiwa amepona.
Nyota huyo
raia wa Uingereza ambaye alishindwa kulitumikia taifa lake katika fainali za
kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil amebainisha kuwa jeraha la goti
lililokuwa linamsumbua linaendelea vizuri na ameshaanza mazoezi ya viungo.
Walcott
mwenye umri wa miaka 25 kurudi kwakwe uwanjani kutasaidia kuimarisha zaidi safu
ya ushambuliaji ya Arsenal baada ya hivi karibuni kumsajili Alex Sanchez kutoka
Fc Barcelona ya nchini Hispania.
Walcott akimiliki mpya kwenye mmoja ya michezo ya ligi msimu uliopita.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment