Pages

Ads 468x60px

Friday, August 1, 2014

VAN NISTELROOY ATEULIWA KUWA KOCHA MSAIDIZI WA TIMU YA TAIFA YA UHOLANZI.





                                         Ruud van Nistelrooy.

Shirikisho la soka nchini Uholanzi (KNVB) limemteua mshambuliaji wa zamani wa vilabu vya Manchester United na Real Madrid  Ruud van Nistelrooy kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa hilo
Nestelorooy ambaye alifunga magoli 35 kwenye michezo 70  aliyocheza katika timu ya taifa ya Uholanzi enzi za uchezaji wake atakuwa akifanya kazi chini ya kocha mkuu mpya wa taifa hilo Guus Hiddink sambamba na  Danny Blind.
Shirikisho hilo la soka la Uholanzi pia limemteua Patrick Lodewijks  kuwa kocha wa makipa akichukua nafasi ya Frans Hoek aliyeungana na Louis  van Gaal kwenda Manchester United huku Patrick Kluivert  akienguliwa katika benchi la ufundi la timu ya Uholanzi.
Katika hatua nyingine shirikisho hilo limewateua Pierre van Hooijdonk, Aron Winter, Sonny Silooy na Michael Reiziger kuwa wasimamizi wa timu za taifa za vijana za nchi hiyo.
                                Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment