Kocha mkuu
wa Chelsea Jose Mourinho ametangaza kuwa mlindamlango namba moja wa timu hiyo Petr Cech huenda akaihama
klabu hiyo msimu huu.
Kauli ya
Mourinho imekuja kukiwa na tetesi kuwa
huenda mlinda mlango wao
aliyekuwa kwa mkopo katika timu ya Altetico Madrid Thibaut Courtois akarejea
kwa matajiri hao wa jijini London.
Imeelezwa kuwa Chelsea ipotayari kusikiliza ofa kutoka PSG iliyoonyesha nia ya kutaka kumsajili Cech huku Morinho akijiandaa kumfanya Mark Schwarzer kuwa mlinda mlango namba mbili baada ya kuja kwa Thibaut Courtois.
Pamoja na Mourinho kukiri Cech yupo tayari kupigania namba kwenye kikosi chake cha Chelsea amesema Thibaut ni mlinda mlango mzuri na chipkizi anayefanya vyema kwenye ulimwengu wa sasa na hilo halina ubishi wowote.
Kwaupande wake Thibaut ameiambia tovuti ya Chelsea kuwa anajisikia furaha kuwa mchezaji wa timu hiyo na anajisikia faraja kubwa kwa mapokezi mazuri aliyoyapata kwenye timu hiyo ya jijini London.
Thibaut Courtois.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment