Pages

Ads 468x60px

Friday, August 1, 2014

UEFA YAANZA UCHUNGUZI GHASIA ZILIZOJITOKEZA KATIKA MCHEZO BAINA YA FC COPENHAGEN NA DNIPRO.


 Shirikisho la soka barani Ulaya Uefa limethibitisha kuwa litanza uchunguzi juu ya  vurugu zilizojitokeza katika mchezo wa hatua ya makundi msimu uliopita baina ya timu ya Dnipro na Fc Copenhagen ambao ulichezewa kuanza kwa dakika 10.

Taarifa ya Uefa imesema uchunguzi huo utalenga sababu za mashabiki kuvamia uwanja mjini Ukrain na kufanya timu hizo kurudi katika vyumba vya kubadilishia nguo kabla ulinzi kuimarisha na pambano hilo kuendelea.

Wakati Uefa ikithibitisha kufanyika kwa uchunguzi huo mkurugenzi mkuu wa timu ya FC Copenhagen Anders Horsholt amesema ghasia hizo za mashabiki zilitokana na tatizo la ulinzi kwenye uwanja wa timu ya  Dnipro.

Katika ghasia zilizojitokeza kwenye mchezo huo takribani mashabiki 30 wa Fc Copenhagen walikamatwa na askari wakiwa na bendera pamoja na  mabango mbalimbali  taarifa hiyo imeeleza.


                                      Mashabiki wa Fc Copenhagen.


    

                         Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment