Mabingwa wa
ligi kuu ya England Manchester City wamefikia makubaliano ya kumwongeza mkataba
wa miaka mine na mshambuliaji Edin Dzeco utakaomfanya aitumikie timu hiyo hadi
mwaka 2018.
Dzeco ambaye
alikuwa amebakisha mwaka mmoja
kwenye mkataba wake wa zamani pamojana
na kuongezwa mkataba ataendelea kulipwa mshahara wake ule ule aliokuwa akilipwa
wa Euro laki moja na themanini na tisa elfu kwa wiki.
Mshambuliaji
huyo ambaye alikiwa kwenye mipango ya kuihama timu hiyo wakati ikiwa chini ya
kocha Roberto Mancin kabla ya kuja kwa
kocha mpya Manuel Pellegrini msimu uliopita alifanikiwa kufunga magoli 26
katika michezo 23.
Dzeco amekuwa mchezaji wa
tatu kupewa mkataba mpya na timu hiyo msimu huu akiungana na Alexsandar Kolarov
na Samir Nasri ambao wamesaini mikataba mipya mwezi wa sita na wa saba mwaka
huu.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment