Kifaa kipya cha Simba -Eliass Maguri.
Hatimae
klabu ya Simba ya jijini Daresalaam leo imekamilisha usajili wa aliyekuwa
mshambuliaji wa maafande wa Ruvu Shooting kutoka mkoani Pwani Elias Maguri.
Maguri
ambaye sakata lake la kwenda Simba lilitawala katika vyombo mbalimbali vya
habari hapa nchini takribani majuma mawili amesaini mkataba wa miaka miwili
kukipiga na wekundu hao wa msimbazi Simba.
Dili
ya Maguri kutua msimbazi limekamilika leo mbele ya makamu wa rasi wa klabu hiyo
ya Simba Geoffrey Nyange ‘Kaburu amesema
wanaimani kubwa na mchezaji huyo kwamba atawasaidia katika miaka yake miwili
atakayokuwa Simba.
Eliass Maguri mwenye jezi ya kijani akiwa mzigoni.
Eliass Maguri mwenye jezi ya kijani akiwa mzigoni.
Mbali
na kuichezea Ruvu Shooting ya Pwani Maguri pia amewahi kukipiga na maafande wa
Tanzania Prisons wenye maskani yao jijini Mbeya.
Kusajiliwa
kwa Maguri ni mwendelezo wa vita ya usajili hapa nchini ambayo itaendelea hadi
katikati ya mwezi huu wa nane mwaka 2014.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment