Kenya na Tanzania zimeshindwa
kufanya vizuri katika michuano ya kufuzu kombe la taifa bingwa Afrika mwaka
2015 huku Uganda ikifanikiwa katika hatua ya Makundi
Lesotho ilitoka sare ya kutofungana
na Kenya mwishoni mwa juma jijini Nairobi, matokeo yaliyofanya Lesotho isonge
mbele kwa ushindi wa goli la kufunga na kufungwa.
Kutokana na kupoteza mchezo huo,
Shirikisho la Soka nchini Kenya limefuta kazi kitengo cha ufundi cha Harambee
Stars , ikiwemo kumsimamisha kazi Kocha Mbelgiji Adel Amrouche.
Kikosi cha Harambee Stars kilikua
chini ya usimamizi wa James Nandwa siku ya jumapili lakini naye alisimamishwa
kazi sambamba na wahusika wa idara ya ufundi.
Mchezo huo uliisha kwa kutofungana
ingawa Kenya ilitawala mchezo wakianza na Victor Wanyama anayoichezea
Southampton na Mc Donald Mariga anayechezea ligi ya Italia
Kenya haikupata upenyo kufuta bao la
Bushi Moletsane lililopigwa mjini Maseru wiki mbili zilizopita.
Mambo hayakua mabaya kwa Uganda
ambayo iliifunga Mauritania 1-0.
Mauritania waliokuwa wenyeji wa
mchezo huo walicheza wakiwa Kumi katika kipindi cha dakika kumi za mwisho baada
ya kuondolewa kwa Karamoko Traore.
Robert Ssentongo alitupia goli pekee
la dakika za majeruhi
Uganda itacheza na waliofuzu kundi E
ambalo limekutanisha Ghana, Guinea na Togo.
Msumbiji ilivuka hatua ya makundi
kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania na kupata ushindi wa jumla wa mabao
4-3.
Mshambuliaji wa TP Mazembe Mbwana
Samatta ailiipa matumani Tanzania kwa shambulio katika kipindi cha pili cha
mchezo lakini Elias Domingues Pelelmbe aliipa ushindi Msumbiji.
Mozambique imefuzu kundi F,
linalokutanisha Cape Verde, Niger na Zambia.
Mataifa 28 watakuwa katika makundi
saba kucheza mwezi Septemba, Oktoba na Novemba ambapo michuano hiyo itaamua
timu gani itaingia kwenye michuano ya kombe la mataifa Afrika mwaka 2015 nchini
Morocco.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment