Monday, August 4, 2014
BARCELONA YATHIBITISHA XAVI KUUMIA MAZOEZINI.
Xavi.
Timu ya Fc Barcelona ya Hispania imethibitisha kuwa kiungo wake Xavi ameumia misuli ya miguu leo jumatatu akiwa mazoezini kujiandaa na msimu mpya wa 2014/2015.
Tovuti ya klabu hiyo imearifu kuwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 34 alilazimika kutoka uwanjani na daktari timu hiyo ndiye atakaetoa taarifa kwamba nyota huyo atarejea lini uwanjani .
Licha ya mara kadhaa kuwepo kwa taarifa kwamba nyota huyo anayeichezea timu ya taifa ya Hispania anaweza kuihama Barcelona msimu huu wa usajili mkurugenzi wa ufundi wa kikosi hicho Andoni Zubizarreta mwezi uliopita alithibitisha kwamba wataendelea kuwa nae.
Kiungo huyo alicheza michezo 29 msimu uliopita wa La Liga nakufunga magoli matatu kisha kuisaidia Barcelona kumaliza katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu ya Hispania nyuma ya mabingwa timu Atletico Madrid.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment