Pages

Ads 468x60px

Tuesday, September 23, 2014

MARTINO AWAITA MESSI, DI MARIA NA KUN AGUERO KUIVAA BRAZIL MWEZI UJAO.



                     Kocha mpya wa timu ya taifa ya Argentina Reardo Martino


Kocha mpya wa timu ya taifa ya Argentina Reardo Martino amewajumuisha nyota hatari wa nchi hiyo kwenye kikosi kitakachoikabili Brazil kwenye mchezo wa Gillette  Superclasico de las America mwezi ujao mjini Beijing.
Katika orodha hiyo kocha huyo amewaita washabuliaji Leonel Messi ,Sergio Aguero  na kiungo Angel Di Maria tayari kwa mpambano huo utakaochezwa tarehe 10 ya mwezi ujao katika uwanja wa Bird Nest.
Katika orodha ya wachezaji walioitwa na kocha Gerardo Martino wamo nyota wa Benfica Nicolas Gaitan,kiungo wa Juventus Roberto Pereyra na mlinzi wa klabu ya  Villarreal ya Hispania Mateo Musacchio.
Michuano ya Superclasico de las America imerejeshwa mwaka 2011 baada ya kutofanyika kwa miaka 35 kabla ya mwaka jana mashindano ya Confederations Cup kufutwa na shirikisho la soka katika bara la Amerika ya kusini.
Kikosi kizima cha Argentina;-

walindamilango: Sergio Romero, Nahuel Guzman.
walinzi: Marcos Rojo, Federico Fernandez, Pablo Zabaleta, Martin Demichelis, Mateo Musacchio, Santiago Vergini.
Viungo : Javier Mascherano, Lucas Biglia, Javier Pastore, Roberto Pereyra, Angel Di Maria, Erik Lamela, Enzo Perez, Nicolas Gaitan.
washambuliaji: Lionel Messi, Gonzalo Higuain, Sergio Aguero.
                               Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment