Friday, September 5, 2014
VIDAL KUIKACHA KAMBI YA TIMU YA TAIFA YA CHILE KWA JERAHA LA GOTI.
Arturo Vidal
Kiungo wa klabu ya Juventus na timu ya taifa ya Chile anataraji kuukosa mchezo ujao wa kirafiki baina ya timu yake ya taifa na Haiti unaotaraji kuchezwa tarehe 10 ya mwezi huu kutokana na kuwa majeruhi.
Vidal mwenye umri wa miaka 27 imeelezwa kuwa anasumbuliwa na maumivu ya goti alililofanyiwa upasuaji kabla ya kuanza kwa fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil ambapo Chile ilifanikiwa kuingia hatua ya 16 bora.
Rais wa shirikisho la soka nchini Chile Sergio Jadue amethibitisha mchezaji huyo kutokuwa kwenye hali nzuri hivyo ataondoka kwenye kambi ya timu ya taifa mara baada ya mchezo wa leo wa kirafiki dhidi ya Mexico..
Rais huyo amesema wakati Arturo Vidal akiondoka kwenye kambi ya timu ya taifa mara baada ya mchezo huo wa leo wa kirafiki wachezaji wengine wataendelea kubaki kambini hapo kwa maandalizi zaidi ya pambano lao na Haiti.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment