Wednesday, September 3, 2014
BEN FOSTER AENGULIWA KATIKA KIKOSI CHA ENGLAND KINACHOIVAA NORWAY LEO.
Ben Foster.
Mlinda mlango wa timu ya taifa ya Uingereza Ben Foster ameenguliwa katika hicho kianachojiandaa kucheza mchezo wa kirafiki leo dhidi ya Norway baada ya kuumia akiwa mzoezini.
Chama cha soka nchini Uingereza FA kimethibitisha kuwa mbali na kuukosa mchezo huo wa leo utakaochezwa kwenye uwanja wa Wembley pia hatosafiri na kikosi cha timu ya taifa kitakachocheza na Uswis juma lijalo kuwania kufuzu michuano ya mataifa ya Ulaya 2016.
FA imesema kocha mkuu Roy Hodgson hatoita mlinda mlango mwengine na badala yake mlinda mlango nambari moja Joe Hart ataendelea na jukumu hilo licha na yeye kusumbuliwa na maumivu ya kidole gumba cha mkono.
Kikosi hicho cha Uingereza leo kitakuwa kikiongozwa na nahodha mpya Wayne Rooney ambaye aliteuliwa hivi karibuni kuchukua nafasi ya Steven Gerard aliyestaafu kuichezea timu ya taifa.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment