Musana
Fahad mwenye jezi ya kijani enzi za uhai wake.
Shirikishon
la soka nchini Uganda FUFA limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji Musana
Fahad anayeichezea timu ya Simba Fc inayoshiriki ligi kuu ya nchini humo UPL kilichotokea
jana jioni muda mchache baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Chelsea na
Manchester City.
Musana mwenye umri wa miaka 24 kifo chake kimetajwa kutokea muda mchache baada ya kiungo wa Manchester City Frank Lampard kufunga goli la kusawazisha kwa mpira wa adhabu na kufanya matokeo yawe goli 1 kwa 1.
Kifo cha mchezaji huyo ambaye imeelezwa kuwa ni shabiki mkubwa wa Chelsea kimehusishwa na mshtuko alioupata nyota huyo kwakuwa jana asubuhi alikuwa mzima wa afya na alifanya mazoezi na timu yake ya Simba fc chini ya kocha Fred Kajoba.
Imeelezwa kuwa kabla ya mchezaji huyo kupatwa na mauti alikimbizwa Hospitali ya Bombo iliyopo nchini humo na taraibu za mazishi yake zinafanywa na klabu yake wakishirikiana na familia ya marehemu.
Mkule.blogsport.com
Musana mwenye umri wa miaka 24 kifo chake kimetajwa kutokea muda mchache baada ya kiungo wa Manchester City Frank Lampard kufunga goli la kusawazisha kwa mpira wa adhabu na kufanya matokeo yawe goli 1 kwa 1.
Kifo cha mchezaji huyo ambaye imeelezwa kuwa ni shabiki mkubwa wa Chelsea kimehusishwa na mshtuko alioupata nyota huyo kwakuwa jana asubuhi alikuwa mzima wa afya na alifanya mazoezi na timu yake ya Simba fc chini ya kocha Fred Kajoba.
Imeelezwa kuwa kabla ya mchezaji huyo kupatwa na mauti alikimbizwa Hospitali ya Bombo iliyopo nchini humo na taraibu za mazishi yake zinafanywa na klabu yake wakishirikiana na familia ya marehemu.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment