Rais wa PSG Nasser
Al-Khelaifi wakati akimtambulisha Laurent Blanc.
Licha ya PSG kuanza vibaya msimu huu wa ligi kuu ya Ufaransa rais wa klabu hiyo Nasser Al-Khelaifi amesema kibarua cha kocha mkuu Laurent Blanc kamwe hakipo hatarini.
Akizungumza baada ya PSG kutoka sare ya kufungana goli 1 kwa 1 na Olympique Lyonnais kwenye uwanja wake wa nyumbani rais huyo amesema wataendelea kuwa na kocha huyo hadi mwisho wa msimu pamoja na mwanzo mbaya walioanza nao.
Pamoja na kukiri kiwango chao cha sasa sio kile kilichotarajiwa amebainisha kwamba ni lazima wapambane kwa nguvu kila siku ili kuwa kwenye kiwango kizuri na wanahakika ya kutimiza malengo ya msimu huu.
Rais huyo amesistiza kuwa mwenendo wa timu hiyo hivi sasa unawakera wachezaji viongozi na wafanya kazi wote hivyo wote kwa pamoja watahakikisha wanacheza vyema michezo inayo fuata ikiwezo wa jumatano ya wiki hii ili kurudi katika kasi yao.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment